Wednesday, May 9, 2012

MAMENEJA-UDSM KUKUTANA KWA CHAKULA CHA PAMOJA HOTEL YA KIFAHARI....

Mameneja - Mwaka wa tatu, kitivo cha Bishara Chuo Kikuu Dar es salaam ( B.COM ) wamepanga kukutana kwa Chakula cha pamoja ( CORPORATE DINNER ) katika Hotel ya kifahari ya MALLIOTE nje kidogo ya mji wa Mabibo.
Wakiongea na Konahabari jana  ( nje ya Cafteria 2 Campus ya mwl. Nyerere - Chuo Kikuu Dar es salaam ) waandaaji wa chakula hicho cha jioni walizungumzia umuhimu wa kukutana pamoja na kujadili mambo ya msingi yanayoigusa jamii kwa namna mbalimbali.
Kwa mujibu wa Paul Venance, mjumbe katika kamati kuu ya uandaaji wa Chakula hicho; Mkutano huo utakuwa na manufaa makubwa kwa wale watakao pata nafasi ya kuhudhia. 
" Hii ndiyo sehemu pekee ambayo mameneja watapata fulsa ya kubadilisha uzoefu na kupeana mikakati yakinifu katika kuzitambua na kuzitumia fulsa zilizopo. Ni sehemu ya kupeana taswira ya soko la ajira na mbinu za kuukabili ushindani wa kibiashara" Alisema Venance.
Corporate Dinner kwa upande mwingine, imetafsiliwa na baadhi ya wadau kama silaha muhimu ya watu kufahamiana na kujenga undugu ambao ndio falsafa mama ya jamii yoyete iliyostaarabika duniani. 
Wadau wanaendelea kutoa michango yao kwa Viongozi - wanakamati walioidhinishwa kisheria kuipokea michango hiyo. SHILINGI ELFU KUMI TU ( 10,000 only ).. ya Kitanzania itamtosha kila Meneja atakaye shiriki katika Corporate dinner kuweza kula, kunywa, kuburudika kwa michezo mbalimbali na kuelimika katika mtazamo wa kimeneja.
Hii Sio ya kukosa, 
                   
PIGA : 0717 438 287            KUWASILISHA MCHANGO WAKO
                                                    WOTE   MNAKARIBISHWA !

No comments:

Post a Comment