Thursday, May 17, 2012

YALIYOJILI BAADA YA KIFO CHA PATRICK MAFISANGO - ALIYEKUWA MCHEZAJI WA SIMBA.

Aliyekua kiungo mkabaji wa Klabu ya Simba Ptrick Mafisango akirushwa juu katika moja ya mechi baada ya kufunga bao wakati wa Uhai wake.

Patrick Mutesa Mafisango alipata ajali saa 9:00 usiku kwenye eneo la Veta na kufariki dunia. Kufuatia kifo hicho rafiki yake mkubwa, Haruna Moshi Boban ameshindwa kuhudhuria mazoezi ya timu ya Taifa yanayoendelea kwenye viwanja vya Karume jijini Dar es Salaam."Alikua akikwepa mtu mwenye baiskeli baada ya kuingia barabarani ghafla wakati gari ikiwa kwenye spidi likamshinda ndipo lilipo tumbukia kwenye mtaro," alisema mmoja ya abiria aliyenusurika kwenye ajali hiyo.

Mchezaji wa zamani wa Simba Boniface Pawasa akilia kwa uchungu huku akifarijiwa na Mchezaji haruna Niyonzima wa Yanga, Pawasa amesema jana walikuwa naye kwenye muziki katika klabu ya Maisha Oysterbay wakati bendi ya Akudo Impact ikifanya onyesho klabuni hapo na marehemu alimuaga kwamba anaenda nyumbani baadae akapigiwa simu kwa simu ya marehemu akiambiwa mwenye simu hii amefariki dunia kwa ajali.

Haruna Moshi Boban akibembelezwa baada ya kutoka kuona mwili wa Rafikiyake marehemu Patrick Mutesa Mafisango kwenye Chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Taifa Muhimbili.

No comments:

Post a Comment