Friday, March 23, 2012

OFISA MAHUSIANO ( DUMA ) AZALIWA…….


Hizi ni picha zilizopigwa usiku wa tarehe 22/03/2012 katika Ukumbi wa London, nje kidogo ya Mabibo Hostel ambapo jopo la wanazuoni kutoka Chuo Kikuu Dar es salaam walikutana kumpongeza Ofisa Mahusiano wa Dar es salaam University Marketing Association ( DUMA ) Bwana Enock Ngulwa  ambaye alikuwa anasherehekea siku yake ya Kuzaliwa.
Bwana Ngulwa aliyejipatia umaarufu mkubwa katika ushawishi na uongozi ndani ya DUMA na taasisi mbalimbali za Kibiashara nchini, alifurahishwa sana na ujio wa wanazuoni hao ambapo alisisitiza umoja na mshikamano wa kijamii katika kufikia malengo. Zaidi ya yote alimshukuru Mungu kwa namna ya pekee ambaye amekuwa msaada mkubwa katika mafanikio yake.

KONAHABARI inamtakia maisha mema na yenye Baraka………
















































No comments:

Post a Comment