Monday, March 26, 2012

MWANAMKE AKIMBIA BAADA YA KUSABABISHA AJALI


Mwanamke mmoja alifanikiwa kukimbia baada ya kusababisha ajali ya gari katika eneo la Mabibo Stand siku ya tarehe 24/03/2012 saa tano usiku. Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo, Mwanamke huyo alionekana kuteteleka na kuyumba kabla ya gari yake aliyokuwa akiiendesha kuacha njia na kuingia katika mfereji eneo la Mabibo Hostel - bara bara inayounganisha eneo la Ubungo na Buguruni ( Mandela road )
               Watu wengi walikusanyika katika eneo hilo kushuhudia kilichotokea lakini hadi kufikia saa sita kamili usiku Mama huyo hakuweza kurudi katika eneo la tukio na hivyo kuwalazimu Polisi kuliondoa Gari hilo katika eneo la tukio saa tisa na dakika kumi na tatu usiku.
                Konahabari   ilifanikiwa kupata picha ifuatayo katika eneo hilo lililotawaliwa na amsha amsha za hapa na pale zikizoonesha mvutano wa kimaslahi kama sio kiuwajibikaji…………….

No comments:

Post a Comment