Saturday, March 31, 2012

DAR ES SALAAM UNIVERSITY ENTREPRENEURSHIP FORUM (DUEF) YAFUNGUA FIKRA CHANYA ZA VIJANA KUJIAJIRI


DUEF imefanya kongamano kubwa na Wanafunzi wa Chuo Kikuu Dar es salaam, Wajasiliamali na Waandishi wa habari. Kongamano hilo limefanyika leo tarehe 31/03/2012 katika nyumba namba b126 jengo jipya la Kitivo Cha Biashara Chuo Kikuu Dar es salaam.
        Maada kuu katika kongamano hilo ni “Ujasiliamali kwa Maendeleo ya Vijana”
       Akiongea na jopo la wanazuoni waliohudhuria katika kongamano hilo Miss ELIZABETH ( mtoa maada katika kongamano hilo) aliwasihi vijana kujiamini na kubuni miradi mbalimbali itakayowawezesha kujiajiri.
         Kwa upande wake aliwashauri Vijana kujiunga na Biashara ya mtandao inayofahamika kama Network Marketing ambayo kwa mujibu wa Elizabeth, biashara hii imekuwa chanzo cha mafanikio ya mabilionea wengi duniani.
ELIZABETH pia hakusita kuwasihi vijana kutumia fursa zilizopo katika kujenga misingi bora ya maisha yao badala ya kusubiri fulsa zitakazopatikana watakapomaliza masomo yao. Akimtumia MICHAEL DELL kama mfano wa kuigwa ( Mmiliki wa kampuni kubwa ya utengenezaji wa Komputer ambaye alifungua kampuni yake akiwa masomoni ). ELIZA alisema inawezekana kwa yeyote aliye na “VISION”
Mtoa maada mwingine katika kongamano hilo ni JOFREY TENGANAMBA – Mhitimu wa Chuo Kikuu Dar es salaam aliyepata umaarufu mkubwa katika tasnia ya utunzi wa Vitabu kikiwemo kitabu cha “KICHWA CHANGU NI HAZINA YA UTAJIRI”.  TENGANAMBA alisisitiza zaidi suala la Vijana kujiamini ili kufikia malengo.
Kushoto ni Miss ELIZABETH akitoa somo

  Imerekodiwa na kuletwa kwako na konahabari- Blog ya kwanza kuifikia hisia yako……

 

No comments:

Post a Comment