Saturday, March 24, 2012

WAHASIBU UDSM WAFANYA KWELI UDBS


Dar es salaam Stock of Exchange ( DSE ) imefanya kongamano na wanafunzi –wahasibu  (Accounting Association of Dar es salaam University- AADU). Kongamano hilo limefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kitivo Cha Biashara Chuo Kikuu Dar es salaam tarehe 24/03/2012.
Kongamano hilo limehudhuliwa na wadau mbalimbali wa mambo ya kibiashara na wanafunzi kutoka idara na taasisi mbalimbali ndani na nje ya Chuo. Kongamano lilifunguliwa mapema na katibu mkuu wa AADU Bwana Daynus Mgaya ambaye aliwakalibisha wageni waliohudhuria katika kongamano hilo.
Mwakilishi  wa DSE na mtoa maada  katika kongamano hilo Bwana MOHAMED KAILWA alipata nafasi ya waelezea wahasibu  na wadau wa mambo ya kibiashara, mambo mbalimbali yahusuyo Dar es salaam Stock of Exchange ( DSE ) ikiwa ni pamoja na njia mbalimbali za udhibiti na ukaguzi wa hesabu.
Bwana KAILWA alitoa maelezo yakinifu juu ya utaratibu wa usajiri wa makampuni katika DSE ambapo alionesha kuongezeka kwa idadi ya makampuni yanayosajiriwa kila mwaka, kwa mujibu wa KAILWA  (DSE ) ilifanikiwa kusajiri makampuni 17 mwaka 2011 ikilinganishwa na idadi ya makampuni 15 yaliyo sajiriwa mwaka 2010 ambayo ni idadi sawa na makampuni 15 mwaka 2009.
Kailwa alitoa ufafanuzi juu ya fulsa zilizopo katika taaluma ya Uhasibu na ukaguzi wa hesabu ( accounting and auditing ) kwamba wahasibu wanayo fulsa nzuri ya kujiajiri katika sector ya ushauri wa mambo ya kibiashara, udhibiti wa fedha, usimamizi wa miradi na ujasiliamali.
Mtoa maada huyo hakusita kuwatahadharisha wahasibu juu ya hasara zitokanazo na udanganyifu katika ukaguzi wa hesabu ambapo, alisema kwamba takwimu zisibitishwazo na wahasibu hutumiwa na taasisi nyingine katika kutafuta fulsa za uwekezaji hivyo basi udhaifu wowote katika sector hii una madhara kwa taifa, wawekezaji na taasisi za kibiashara.
                KONAHABARI ITAENDELEA KUWAJULISHA MATUKIO MBALIMBALI…………………….
 KAILWA AKITOA SOMO


 KULIA NI OFISA MAHUSIANO WA DAR ES SALAAM MARKETING ASSOCIATION ( DUMA )




 KATIKATI NI KATIBU MKUU WA AADU BWANA DAYNUS MGAYA

No comments:

Post a Comment