Friday, March 30, 2012

TAARIFA YA MSIBA KUTOKA KATIKA FAMILIA YA NDUGU SHIRIMA


Familia ya Ndugu Shirima wa Moshi wakiaga mwili wa mpendwa wao  Francis Shirima.
Marehemu Francis Shirima ni Baba mzazi wa Beatrice ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu wa kitivo cha Biashara Chuo Kikuu Dar es salaam. Safari ya kumuaga marehemu Francis Shirima ilianza mida ya saa sita mchana ambapo wanafunzi wa Kitivo Cha Biashara walioonekana kuwa na nyuso za huzuni walianza kujikusanya katika eneo la Kontena tayari kwa safari ya kwenda kanisani.
Misa ya kumuaga marehemu Francis ilifanyika kwa mujibu wa taratibu za kanisa zilizopewa kibali mbele za Mungu kwa ajiri ya sifa na utukufu wake.
Msemaji wa familia kwa niaba ya familia, ndugu na jamaa alitoa shukrani za dhati kwa Watu, taasisi na jumuiya mbalimbali zilizo husika kwa namna moja au nyingine kushirikina nao katika msiba huo.
Msemaji alipata nafasi ya kutoa historia fupi ya Marehemu ambapo alisema “Marehemu Francis Shirima alizaliwa mwaka 1956 katika wilaya ya Moshi – Mkoani Kilimanjaro. Alijipatia Elimu yake katika Shule mbalimbali kabla ya kuanza kujihusisha na shughuli za kilimo na Biashara.
Marehemu alikuwa akipata matibabu katika Hospitali mbalimbali ndani na nje ya nchi zikiwemo Hospital ya Agakani  na Hospitali ya taifa ya Muhimbili.
Mwili wa marehemu umesafirishwa kwenda Moshi kwa Mazishi, Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahali pema peponi….!
            Imerekodiwa na Konahabari…..
 Watu wakiingia kanisani 

 msemaji wa familia ya Shirima akitoa historia fupi ya marehemu
 watu wakitoka kanisani baada ya misa ya kumuaga marehemu

 mwili wa marehemu unaingizwa kwenye gari

 Watu wakiangalia msafara wa gari zilizoondoka kumsindikiza marehemu

No comments:

Post a Comment