Sunday, April 29, 2012

MWANA-CHADEMA ALIYECHINJWA ARUSHA NI PIGO KWA TAIFA......

Msafiri Mbwambo miaka 32 ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kata ya Usa-River, wilayani Arumeru mkoani Arusha, ameuawa kinyama kwa kuchinjwa na watu wasiojulikana.
Tukio hili limetokea wakati nchi ipo katika wakati mgugu wa kutafakari hatma ya umasikini wa walio wengi na umuhimu wa kupunguza (gap) kati ya walionacho na wasionacho. Umuhimu wa kupata Viongozi Bora watakao tunga sheria zinazo weza kudhibiti mianya ya Rushwa na Ubadhilifu wa mali za umma kwa maslahi ya kizazi kilichopo na kijacho.
Mbwambo aliuawa na watu wasiojulikana baada ya kupigiwa simu kumwita majira ya saa mbili usiku, wakati akitazama taarifa ya habari eneo la Mji Mwema akiwa na watu wengine.
Katibu wa Chadema wa Wilaya ya Arumeru, Dotnan Ndonde, alisema mara baada ya marehemu kuondoka muda mfupi baadaye, mwili wake uliokotwa eneo la Shule ya Mukidoma, Kusini mwa mji wa Usa-River umbali wa takriban kilomita mbili kutoka alipokuwa.
“Tulimkuta akiwa anavuja damu ilionekana muda si mrefu alikuwa amechinjwa na watu wasiojulikana ambao walikuwa wametoweka,”alisema Ndonde

Wapenzi na Wanachama wa Chama Cha Democrasia na Maendeleo ( CHADEMA-Chuo Kikuu Dar es salaam) wamelaani kitendo hicho na kudai kuwa kitendo hicho ni kinyume kabisa na haki za binadamu.
Kwa upande wao baadhi ya viongozi wa CHADEMA hawa kusita kotoa hisia zao kuhusiana na tukion hilo la kinyama Arusha.
Ndonde alisema kwa mazingira ya tukio na hali ya kisiasa eneo la  Meru, anashindwa kuyatenganisha mauaji hayo na siasa.
Mbunge wa Arumeru Mashariki kupitia Chama Cha Democrasia na Maendeleo ( CHADEMA ) Bwana Joshua Nassari ameeleza kusikitishwa kwake na tukio hilo la kinyama na kusema kuwa bado joto la kisiasa lipo juu wilayani humo na zaidi amelitaka Jeshi la Polisi kuhakikisha linawasaka na kuwashughulikia ipasavyo wale wote waliohusika na mauaji hayo.

No comments:

Post a Comment